Wednesday, April 20, 2011

Wake up Africans! 'Bodies thrown into wells' in Nigerian riots

Youths stage running battles with soldiers in Nigeria's northern city of Kano shortly after the annoucement …


KANO, Nigeria (AFP) – Post-election riots in northern Nigeria have left many dead, thousands displaced and hundreds wounded amid claims that bodies had been thrown into wells in areas hit by unrest.

Nigerian President Goodluck Jonathan called on political and religious leaders to condemn the violence over his election victory, adding that most of the rioters appeared to be "unemployed young people".

He pledged that the government would work to change their situation "so that they will no longer be tools for people to use".

Fearing reprisals, authorities have not given a death toll for the rioting that began sporadically during the weekend over allegations of vote rigging and quickly spread to some 14 states on Monday. Officials have however spoken of many killed.

An estimated 25,000 have been displaced and some 375 wounded, according to the Red Cross. Police said dozens of people had been arrested.

"Things are relatively calm right now, but violent protests went on last night, especially in Kaduna, Katsina and Zamfara (states)," Umar Abdul Mairiga, the Nigeria Red Cross disaster management coordinator, told AFP.

"What may come out of there is not very palatable because many people were killed, especially in southern Kaduna. The displaced people are getting hostile because nothing is coming up in terms of relief."

Tuesday, April 19, 2011

UBINAFSI

UBINAFSI umekuwa ni janga la dunia nzima, si Amerika si Ulaya si Asia, lakini kwa hapa Afrika janga hili linaonekana kushamiri zaidi kuliko sehemu zingine za dunia.

Ubinafsi, tabia ambayo imo ndani ya mtu mmoja mmoja umekuwa ni tatizo kubwa linalokwamisha maendeleo katika ngazi zote kama familia, jamii na taifa.

Ubinafsi hapa nchini umekuwa ni ugonjwa mbaya ndani ya baadhi ya watu na una athari katika nyanja muhimu katika jamii, hivyo unahitaji kupigwa vita na kila mpenda maendeleo ya nchi yetu, kwani tusipoupiga vita basi tutaendelea kuwa maskini huku wachache wakineemeka.

Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere hata kabla ya Uhuru alikuwa ameshajua kuwa Taifa lina maadui wabaya watatu, umaskini, ujinga na maradhi, hivyo aliamini Taifa haliwezi kuendelea bila kuwapiga vita maadui hao hata kama nchi itapewa uhuru wake, Hivyo baada ya uhuru alitangaza vita ya mapambano kuwatokomeza maadui hawa.

Wengi tunafahamu mafanikio ya vita hii na mojawapo hakukuwa na tofauti za kimaisha katika jamii. Naamini adui ubinafsi alikuwepo sana tu ila hakuweza kujidhihirisha waziwazi pengine kwa kumuogopa Mwalimu. Naamini pia adui huyu alifanya kazi kwa siri kubwa na kadri siku zilivyozidi kwenda aliota mizizi.

Mwalimu alipotutoka tu, adui akaanza kujidhihirisha wazi wazi,aliyekuwa amevaa mavazi ya kondoo kumbe alikuwa ni mbwa mwitu na huwezi amini hata baadhi ya watumishi na kondoo wa Mungu wamegeuka mbwa mwitu.

Watu wengi leo hii hasa wenye dhamana mbalimbali na wanaotuongoza ni wabinafsi wa kutupwa wasiojali maslahi ya walio wengi. Badala yake wanajiangalia wao na makundi yao kwanza.

La kusikitisha zaidi hata yale mawazo ya kukumbuka kuwa kuna makundi mengi ya watu katika jamii wanaohitaji mahitaji maalumu yani wasiojiweza na pia kwamba asilimia kubwa ya jamii ya watanzania inaishi katika maisha ya kifukara hawana. hata kama wanaikumbuka jamii basi ni kama vile wanasema shauri lao.

Mifano ipo mingi sana, kwa mfano maamuzi juu ya masuala yanayowagusa walio wengi sio jambo geni kusikia kiongozi fulani anaamka tu asubuhi na kutoa matamko ya maamuzi nyeti bila kuwashirikisha wataalamu na wadau mbalimbali matokeo yake maamuzi yake yanaonekana hayana tija kwa jamii.

Wasomi wetu na viongozi wetu leo hii wengi hawana habari tena ya kuitumikia jamii, wao wanaangalia maslahi yao, matumbo yao na familia zao. Mikataba mingi ya uwezekaji unakuta imesainiwa kwa kuangalia zaidi maslahi yao binafsi na sio maslahi ya jamii ya watanzania. Nani asiyejua swala la kujilimbikizia mali isivyo halali? Nani asiyejua maswala ya rushwa na ufisadi,nani asiyejua matumizi mabaya ya pesa za walipa kodi.yote haya sababu tu ya ubinafsi.

Viongozi wetu wengi leo hii wako tayari na wanaona ni haki yao kutumia pesa nyingi za walipa kodi vibaya kwa kununua magari ya kifahari ya gharama kubwa kila mwaka wakati jamii hiyo ya walipa kodi ina matatizo mengi yanayotatulika.

Inashangaza kuona hata Wabunge wetu, wawakilishi na watetezi wa wananchi Bungeni miaka ya hivi karibuni wamekuwa mstari wa mbele kudai waongezewe maslahi zaidi utafikiri hizo pesa wanakwenda kuzigawa kwenye majimbo yao. Hili limefanya hata mtu awe tayari hata kumuua mwenzie kwenye mbio za Ubunge ili yeye apite.

Katika upande wa familia, utakuta mtu ana uwezo mkubwa tu na watoto wake wanasoma hata Ulaya, lakini yeye kuwasaidia hata ada ya masomo watoto wa ndugu zake wasio na uwezo anaona shida, anaona shida hata kuwapa mtaji ndugu zake wasio na uwezo sababu ya ubinafsi, yeye anajali na kuangalia familia yake basi.

Zimwi hili la ubinafsi limekuwa likikwamisha maendeleo kuanzia ngazi ya familia hadi katika taifa, hivyo basi hatuna budi kulitokomeza lakini pia viongozi wa dini wasimamie hili kwani hata katika vitabu vitakatifu ubinafsi umekatazwa.

Chanzo: Mwananchi, Thursday, 17 February 2011 19:56

Amani na Upendo

Monday, April 18, 2011

UNKNOWN


Dr. Martin Harris awakens after a car accident in Berlin to discover that his wife suddenly doesn't recognize him and another man has assumed his identity. Ignored by disbelieving authorities and hunted by mysterious assassins, he finds himself alone, tired and on the run. Aided by an unlikely ally, Martin plunges headlong into a deadly mystery that will force him to question his sanity, his identity, and just how far he's willing to go to uncover the truth.
Cast & Crew
Starring:

Liam Neeson (Dr. Martin Harris)
January Jones (Elizabeth Harris)
Diane Kruger (Gina)
Aidan Quinn (Martin B.)
Frank Langella (Rodney Cole)
Bruno Ganz (Jurgen)
Sebastian Koch (Professor Bressler)
Mido Hamada (Prince Shada)

Directed By:
Jaume Collet-Serra
Genres: Drama, Thriller and Adaptation
Running Time: 1 hr. 49 min.
Release Date: February 18th, 2011 (wide)
MPAA Rating: PG-13 for some intense sequences of violence and action, and brief sexual content.
Distributors:
Warner Bros. Pictures


the movie is among gud staff this 2011. must wotch it!

YEAR OF GENTLEMAN!










THIS happened when your so so inlove with Fashion! the guy is so superb in art, fashion n` design. It’s a bit of a find when you come across a designer with a fresh yet wearable take on men’s clothing. Big up Haki Ngowi.for more check out here

Friday, April 15, 2011

KATIBA

Mungu akasema, Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu, wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. Mungu akamuumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu akamuumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kitambaacho juu ya nchi.


Kwa waamini kwamba wameumbwa na Mungu, mungu hakumpa mwanadamu mamlaka ya kutawala mwadamu mwenzake. Katika kundi kubwa la watu au wanyama hatuwezi wote kuwa mbele, ni lazima wachache kati yetu tuwatangulize kama wawakilishi wetu kwa kufuata taratibu tulizo ziweka sisi wenyewe wana kundi au wana jamii fulani. Taratibu ambazo kila mwanajumuia ameridhika nazo na hana shaka ni kwa manufaa ya kila mwanajumuia. Taratibu hizo zitaridhiwa na wote wanaotaka kutuongoza ili tufikie pale ambapo wote tumetazamia kufika bila kuwa na manung'uniko yoyote kwa wale wa mbele na wale wa nyuma.


Kuweka taratibu ambazo zitaridhiwa na kila mwana jumuia ni kazi ngumu na inahitaji utulivu mkuu. Kila kiumbe anamaono tofauti, kila kiumbe ana nafsi ya kipekee, makubaliano ya viumbe wenye hulka tofauti yanahitaji utulivu wa mkubwa na mdogo, mwanamke na mwanaume, vijana na wazee. Mchanganyiko wa wanawake na wanaume, vijana na wazee unaweza kuwa ndio mchanganyiko utakao leta manufaa ya makubaliano ya taratibu za kuendesha jumuia husika. Pasiwepo mjuaji wala tamaa ya kitu fulani katika kuandaa kitu cha manufaa ya jumuia kwa muda mfupi au mrefu.


Kulinda na kuenenda kutokana nataratibu ambazo jamii fulani imeziweka ni jambo la lazima katika jamii hiyo. Mtu aliye yote anapo kiuka taratibu hizo ataadhibiwa kutokana na taratibu hizohizo ambazo jamii imeziweka kwa maslahi yao wote.


Taratibu za maridhiano ya viongozi na waongozwa uitwa KATIBA. Si kazi rahisi kuandaa katiba mpya itakayo ridhiwa na watu zaidi ya milioni 40 kiurahisi. Katika kuandaa katiba kila mwanajumuia anatakiwa kushiriki vyema maana katiba ni mali ya watu wote wa jumuia fulani. Jumuia inayofanikiwa kuandaa katiba iliyoridhiwa na watu wengi katika jumuia hiyo ni jumuia yenye mafanikio, ni jumuia ya upendo, ni jumuia mtu kwa watu na watu kwa mtu kwani ni kwa ajili ya manufaa ya wote. Kazi ya uandaaji wa taratibu za kuendesha jumuia ya watu zaidi ya milioni 40 yahitaji muda na busara kuu.


Kutoa muda wa siku nne kuchangia maoni ya muswada wa katiba mpy ya jamuhuri ya muungano ni kichekesho. Watawala nao yaelekea hawajui nini maana ya katiba. Pupa pupa ifanye kwenye maisha mengine na si katika kuandaa katiba. Katiba haitungwi kwa ajili ya watu waishio mijini pekee, hapana, katiba ni ya watu wote wa mijini na vijijini. Tumesikia sehemu zilizo tumika kupojea maoni juu ya muswada wa katiba mpya, katiba kwa ajili ya Jamuhuri ya muungano wa tanzania. Ni mijini, hakuna watu wa kuchangia chochote waishio vijijini, hii ni hatari. Katika katiba hakuna masikini na mkokoteni wake au tajiri na gari lake. Katiba mali ya wote, hivyo kila mwanajumuia, mjini au kijijini, msikitini au kanisani anatakiwa kushiriki vyema katika uandaaji wa katiba.


Watanzania washikamane wawe imara katika kuhakikisha yale yote ambayo yameonekana ni mapungufu ya jumuia yetu kutokatana na katiba iliyopo yanaondoka na kupata katiba mpya na safi kwa manufaa ya mla mkate hotelini na mla muhogo shambani. Kuhakikisha katiba inakuwa wazi katika uwajibikaji wa kila mtanzania, katiba isiruhusu kuwepo miungu watanzania ambao hata akikunyea mdomoni huna kwa kumpeleka, hapana!


Mtoto tumboni na hata mababu vitandani waheshimike katika mchakato wa kuandaa katiba mpya. Kazi ni ngumu lakini kwa kushirikiana vyema tutaiweza kwa ufanisi mkuu. Tuseme hapana kwa wale wenye nia ya kuweka taratibu fulani kwa manufaa yao, hawa ni watu wabinafi, tuwakatae kabisa!


Mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe. Jenga nchi yako kwa kuhakikisha inapata katiba mpya na imara, kuwa imara na mwenye busara katika kusimamia hilo.


Amani na upendo.

Thursday, April 14, 2011

DAMU INA RADHA TAMU

Damu kitu ni aghari sana. Hakuna hasiye tambua huwezi ishi bila damu. Damu ni muhimu kwa afya nzuri kwa kuwa mwili unategemea damu isukume oksijeni na viambatanishi vingi ili weza zifikia seli zake. Moyo hufanya kazi ya kusukuma damu lakini hauwezi ishi pasipo damu. Damu inabeba caboni dayoksaidi na taka mwili nyingine kupeleka kwenye mapafu, kibofu na kwenda kwenye mmeng'enyo wa chakula ili viweze tolewa nje ya mwili kama taka mwili. Pasipo damu tusinge weza pasha wala pooza miili yetu, tusingeweza pambana na magonjwa na wala tusingeweza toa taka mwili. Damu inathani kubwa.

Kila kitu chenye thamani mwilini au ardhini, mjini au porini, kwa mtu au mnyama uhitajika na mtu, ardhi na wanyama pia. Watu wanadamu katika miili yao na inapopungua wanaongezewa ikipatikana, wanyama pia vivyo hivyo. Ardhi haina damu kama damu ya mtu au myama lakini inapenda sana damu ya mtu au mnyama kwa kuwa damu ni tamu.

Ardhi ikionja damu haichoki kuhitaji hitaji hilo tamu. Ardhi niishiyo imeonja na sasa imezoea damu. Kwa kuwa mchovya asali hachovyi mara moja basi ni vigumu kwa ardhi ya nchi yangu kuikana damu tamu tena damu ya watu.

Msitu wa pande damu ilimwagika wazi hilo twalijua, Dito aliipa ardhi inachokitaka wazi bila kuogopa, zanzibar watu wakauana tukapata wakimbizi, wakulima na wafugaji kuilisha ardhi tamu yake kila kukicha, Arusha yakatokea ukweli mewekwa kwapani, machweo na mawio yakafika Madale ardhi kupigania damu nyingi na tamu kwa ardhi mwagika. Mtanzania mpenda amani na haki alikuwepo jana leo hapana kesho kitendawili. Watu wanajichukulia sheria mikononi kuchinja wevi na maisha yaendelea. Jazba haina utu. Chochoko ya ardhi kutaka damu haitaisha kwa kuwa imeshazoea sasa na itafitini kwa kila namna ipate tamu ya damu.

Mtanzania kupiga na kuua mtanzania mwenzake si jambo baya na wala hajutii. Anafurahi na kushaingilia na kuendelea na maisha pasi na wasi. Thamani ya maisha ya mtu mwingine kwa mtanzania wa chini na hata wa juu haipo. Waliomwaga Damu pande ni viongozi walo aminiwa na kupewa vyeo katika taifa letu na waliomwaga damu madale ni masikini kama mimi. Ardhi inataka Damu.

Kiu ya ardhi ikiwa kuu ni majuto. Pitia simulizi za vita ya Kimbali Rwanda, pitia simulizi za somalia na nchi nyingi ambazo hazikuona thamani ya mwingine katika maisha na kujiona wao ndio bora zaidi. Kabila kwa kabia, dini kwa dini, masikini kwa tajiri, tabaka kwa tabaka, ardhi haina shaka uaneni ipate shibe, inywe damu tamu ishibe.

Sintoishangaa Tanzania ya vita, kwani utu si kitu kwa raia wa tanzania. Madale watu wameuana kwa panga na marungu tena kwa kuangaliana usoni bila shaka yoyote nini kumpiga yule wa dini fulani au chama fulani?

Damu ina radha tamu. Mungu apishe mbali kiasi cha damu ardhi ya tanzania ilivyo kunywa kiwe chatosha. Awajalie watanzania utu wa kujali utu wa watu wengine, azijaze nyoyo za raia wa Tanzania ujasiri wa kuchukia sheria mikononi, watu watumie madaraka yao kwa matakwa ya wote, wakimbie rushwa, wapendane na kujua sisi wote ni ndugu, tabaka fulani na tabaka fulani, dini fulani na dini fulani Mungu wetu ni mmoja.

Damu ni tamu na ardhi inahitaji damu nyingi. Tusipojali utu tutapigana, tutauana na hakuna jema litakalo tufika.

Amani na Upendo.

afrotanza gallery