Monday, November 29, 2010

Wivu wa chuki!

Jazba hainisaidii duniani. Wivu wa chuki ni aghali maishani. Nikahitaji nini kushiriki na huyu katika kufanikisha maisha huru ya watu wengi? Nijikombe vipi kwa ng’ombe anipaye kwato ninyonye damu? Nitaruka vipi na mbayuwayu wenzangu hili khali nimenyonyolewa mbawa na manyoya yote lowana? Dunia haiishi maajabu. Maisha ni changamoto, changamoto ngumu na zenye kubadilika kila sekunde. Maisha ni mchezo wa mapambano, cheza vizuri, cheza sana kwa bidii yako yote lakini tambua leo utashinda kesho utashindwa. Usikate tamaa na wala usijitenge na timu yako nzuri yenye ubunifu ukadhani kwamba kuna timu ishindayo siku zote, hakuna.

Adui wapo na rafiki pia. Nani rafiki yako mkuu? Mtu fikirika matendo yangu ni fumbo, rafiki yangu mkuu ni mimi mwenyewe. Kushiriki au kutoshiriki kitu na yule au wale si kitu katika kukamilisha karama na kalamu yangu. Kama hawa hawataki kuwa nami basi wale watakuwa nami na ni wazi siwezi ishi pasipo wewe au wao, adui au rafiki. Nikiwa peke natembea nafurahi sana kwani mimi katika mimi ni kiumbe kamilifu. Nikiwa nanyi sintokuwa mjuaji katika ninyi kwani mimi katika ninyi nina mapungufu mengi.

Umoja ujenga imara ya kitu na utengano udhoofisha juhudi ya jumuia ya watu na kuleta kitu dhaifu. Umoja wangu na wanyonyaji hauna tija zaidi ya kunyonya wengine zaidi na kunyonywa mie nikadhoofu. Umoja wangu na wanye haki ni heri na fanaka ya maisha yangu na wengine wengi. Kwa hilo sintoenda katika shauri la wasio haki. Nitashiriki vipi na rafiki niishie nae chumba kimoja ili hali ana kula pamoja na wasio haki? Mie mtu wa haki, naogopa shiriki na yule hasiye haki kwani wengi huwa na jazba katika kuongelea haki na kushikiria imani isiyo nyonyaji.

No comments:

afrotanza gallery