Thursday, April 22, 2010

NITAKUWA KIPOFU MPAKA LINI?

Kweli kipofu hawezi mwongoza kipofu. Hata ningekuwa wa hali ipi siwezi lenga kile nisicho kiona na nikifanya hivyo nitakuwa sitambui kama ni nini nimekifanya na kwa manufaa gani.

Jongoo hakujaliwa vaa saa lakini ana busara sana ya kutambua muda na kuutunza. Mimi sielewi majira ya maisha yangu, sijui ni wakati gani niwike na wakati gani nitulie, wakati gani nitafute na wakati gani nile na kupumzika.

Mimi mwanadamu nimekosa nini na wala nisifanikiwe katika maisha yangu? Je! Mungu anaupendeleo? Iweje wengine wafanikiwe mimi niishi kwa manung'uniko?

Yamkini ipo sababu. Tunaambiwa tuwaangalie ndege wa angani hawalimi na wala hawavuni lakini wanaishi. Niwe wa aje niishi maisha ya viumbe visivyo na utashi?

Basi kama hivi ndivyo, mimi kiumbe mwenye utashi sijitambui. Kiumbe nisiye jitambua siwezi fanya kitu chochote chenye manufaa kwangu na kwa jamii yangu. Kuto kujitambua kunanifanya niwe mtumwa, nitegemee mawazo ya watu wengine, nisiwe na maamuzi imara juu ya fikra zangu, nisijue majira ya mwaka wa maisha yangu na wala nisiwe na mvuto kwa maendeleo yangu kihali na kiakili.

Kuto kujitambua kunanifanya niwe muoga, nisijiamini na wala nisiaminiwe, nijawe wivu mkuu na kuwa mtu akili raruka.

Kuto kujitambua kunanifanya niishi maisha ya kusadikika na kuto eleweka. Nisitambue wakati gani napanda na wakati gani nashuka, wakati gani nikimbie na wakati gani nisimame.

Kweli kutokujitambua kunanifanya niwe kama maji. Kwamba umbile langu lategemea birika lililo nibeba. Niwe mtu wa kukimbia tu na nisitembee hata siku moja!

Ndio vidole havilingani, nami nisingependa vilingane. Mungu aliumba usiku na mchana kwa maneno, usiku na mchana viwe. Ikawa usiku na ikawa mchana. Nini maana ya maneno haya kwangu?

Mimi sikujaliwa karama? Mimi sikujaliwa busara? Mimi sikujaliwa maono? Mimi sikujaliwa uchaji?
Mimi sikujaliwa akili?

Kama Mungu aliya niumba alinijalia hivyo na kunipa miti na matunda ya kula iweje niwe masikini? Nitaishi na umasikini mpaka kifo changu? Utungu wa namna gani huu? Au huu ni msalaba wangu niwaokoe watu wa ulimwengu fulani nisio ujua? Yesu aliubeba msalaba kuokoa watu wa dunia hii, mimi ninabeba msalaba huu wa umasikini kumuokoa nani?

Ni kipofu. Nasema tena mimi ni kipofu. Natamani nione na niishi maisha ya mvuto katika nafsi yangu. Natamani nitoke gizani na iwe mchana kwangu, natamani nijitambue na nitambue majira ya maisha yangu.

Machozi yananitoka, nitakuwa kipofu mpaka lini?

Tuesday, April 20, 2010

THE VALUE OF WOMAN



THE VALUE OF A WOMAN

The value of a woman is more than jewellery, those in marriage should keep that in mind and husband must be aware of that his wife experience needs to be esteemed and recognized in her value and mission as a woman.
When it comes to conjugal harmony it depends a great respect for the interior and spiritual side of a woman. The feminine natural is a most sensitive recorder of facts and person. A woman can suddenly become meditative and perplexed over the remembrance
Of a particular morning, an all ill-fated day, a past sallow, recalled even just by the tone of voice of the person speaking to her or because of the different manner in which someone gazes at her.

As a husband keep in mind that flower may be beautiful even without fragrance, but fragrant flower is twice as beautiful, likewise a gruff husband may be good but good and gentle husband is twice a treasure.

There are little things in marriage that can make one of the spouse or even both live in the word of “I wish I could knew I could not have got married to you” you might ask yourself why are so many heart break in a relationship and in marriage?
The only secret that most fail to understand if not to put into practice is always a man should be grateful to his wife for all that she is and for all that she does, a man can use a trick in winning her wife `s heart by praising her using sweet words.

What is wrong if a man tells his wife you are the mirror in which I see my self, you are my heart, my light, my life, the object of my happy hours, strength in my labour and my hope in my troubles. To make it sound sweet a man can add “you are the wing by which I can fly toward better things and you are for me the angel who carries me towards the light of God.
Do we say that when men are looking for a lady to marry they shouldn’t be lured by facial appearance? Instead they shouldn’t consider a various noble – woman is worth more than a rubies of which her husband has full confidence in her and lacks nothing of value.
She is someone who can bring good to a man and not harm all of the days of a man’s life. She select wool and flax and works hard towards achieving success and her husband has full confidence in her and lucks nothing of value, bring good and not harm all of the days of their life in marriage. A woman who gets up while it is still dark, she provides food for her family.

A man must remember that the woman is also concerned about fashion, cleanliness, and elegance. If a man’s temptation is the woman, her temptation is jewels, lovely things.

A good husband should be able to love is wife also in little things. The women loves small details and want to be the center of affection and attention, at least once in while it is a good thing for husband to praise his wife for something well done, to recall her acts of virtue, to praise her success deeds and personal accomplishments, to lay stress on the fact that without her, his life will be without shine, enthusiasm and joy.

Remember a woman is like bee if well treated it gives honey, if neglected and mistreated she stings. Above all there would be no harm to say pardon whenever he realizes he has done something wrong. The best remedy for a fault is to recognize one’s own mistakes.

Wednesday, April 14, 2010

Sean Kingston for 2010 Kilimanjaro Music Awards

in Tanzania kilimanjaro music award 2010 at Diamond jubilee hall Dar es salaam, the teen rap / reggae star of jamaica SEAN-KINGSTON will perform on 14th and 15th of may!

Monday, April 12, 2010

MIMI NA WEWE WOTE WEHU!

MIMI NA WEWE WOTE WEHU!

Pole mwehu mwenzangu kwa uvumilivu ndani ya basi letu, basi lililo na viti tusiweze vikalia, basi lililo na vioo tusiweze vifunga, basi lililo na taa tusiweze ziwasha, basi lililo na saa pia tusiweze tambua muda.

Pole kwani faida tuipatayo ni kusimama safari yetu yote mpaka kituo hiki, kituo cha kuchagua dereva na kondakta mwingine, hatukuweza funga vioo na matokeo yake vumbi, jua, na mvua vimekuwa vyetu safari nzima, usiku mchana pia tumekuwa buruzwa kwani hawakuweza washa taa za basi letu kuona wapi tulipo na wapi twaelekea, safari yetu imekuwa ngumu kwani hatukutambua majira ya siku, wiki, mwezi na hata mwaka.

Ninafuraha kuu kwani sisi hutuna tabia ya kulalamika, sisi ni wapole tusiopenda kelele na tumekuwa wanyoofu kwa kuinama chini kama kondoo.

Tulipo ianza safari yetu walituhadi mengi, mengi kweli walitutamkia. Hawakuwa na woga wowote, walituambia watatuwezesha tuweze kaa na kustarehe ndani ya basi letu, watafunga vioo na kuwasha AC ili tusinzie kama tuko peponi, kwamba watawasha taa pindi tutakapo taka ona ili sisi pia tuelewe muelekeo wa basi letu, watawasha taa ili tuweze ona pindi kiza kitapo wadia, kwamba saa itaheshimiwa kwani watatusomea na kuzingatia muda kadri ya matakwa yetu na walituahidi kulilinda basi letu kwa wavamizi na wezi wa ndani na nje pia .

Pole kwamba tumefika hapa wao mwenyewe hawatambui kwanini wameshindwa kamilisha yale walio tuahidi, maisha bora kwa kila abiria na hawaelewi kwa nini basi letu ni bovu. Wanajua na ukondoo na aibu zetu tunawaangalia kwa jicho la chinichini, tunashindwa tamka kwani tabasamu zao ni mvuto sana kwa wengi wa wehu wenzetu. Wanatambua wameshindwa kutuweka bora tukae tutulie tufaidi safari yetu na kukuacha tuteseke, tutoke jasho na tunuke ujinga.

Sisi ni watu wazuri sana, hata tukichomwa sindano hatushituki, tumeridhika na hali duni ya basi letu, tumeridhia vifaa vya basi letu chukuliwa na wapita njia, buzwagi nyamongo pia sisi hatujalalama, tumeipenda staili ya sisi potezwa njia na kuingia njia zilizo tugharimu pesa nyingi kama njia za rites na tics.

Sisi kweli ni wavumilivu, twapaswa jisifu. Ingawa wao na wahudumu wao wengi wanatope, wamechafuka. Wamechafuka kwa kushikana mikono na wale wachafu au kushiriki kuogelea kwenye tope. Tunawavumilia kukaa nao ingawa wananuka uvundo, hatujawachoka kama ilivyo kawaida yetu.

Wanatambua kuwa wanakashfa mbali mbali, sisi tumenyamaa na kuwapa sifa na kuwapigia makofi kwa mwendo mbaya na kutuburuza vyema. Wao kweli wanatuunga mkono kwani kashfa zao kwetu sifa. Wanatambua kati yao kuna mafisadi, wanachekelea na sisi na wehu wetu tumewaunga mkono katika kicheko hicho na kuwaacha waendelee kufaidi na kutunyonya vilivyo. Wanatupa pongezi nyingi, hatuna wivu na tuna uvivu kichwani. Masikio tumeweka pamba, wanao wasema waseme na usiku watalala na sisi endelea buruzwa na basi bovu kama lilivyo.

Imeongelewa BOT kuna wizi, tumewafurahisha kwa ukimya wetu katika hilo. Inapendeza kwani tuna busara na tunatambua kuwa BOT hela haziishi. Hata kama zitaibwa saba mara sabini. Ikaja Richmond na sera zake za unyonyaji na udanganyifu, hayo wamepiga zile tiktaka na kutupiga bao, hatukuelewa hata mpira umetupitaje, wametupiga bao na kutufumba midomo, sisi pia tumefumba pasi na shaka, tena tumeridhia ujanja ujanja wao.

Wamenunu rada ili wawe na uwezo wa kuzuia kunguru wasinyee basi letu, tena bila sisi wenye basi toa maoni yetu na vipaumbele katika safari yetu, ikatambulika kuna rushwa katika hilo. Walicheka wakigonga glasi zao, tena sana kwani tuliwafurahia na kuwashangaa waongeleao rushwa, hata kama kuna rushwa kwani sisi wehu tumepungukiwa nini? Hii ndio rangi ya basi letu, halijachafuka na sisi tumesha izoea rangi hii.

Wehu wenzetu wakapanua midomo kupayuka hovyo kuwa, kuna abiria wameamishwa sehemu zao kumpisha mzungu. Wao wakatabasamu na kutamka yaani uache mtu mweusi atambe wakati mzungu kaja? Wakaendelea tukebehi kuwa lini tutajifunza kizungu kama hatuta kubali wehu na wachovu wenzetu waache sehemu zao na kuwaachia wazungu nafasi nzuri na kubwa za kutosha? Mzungu nae katia sumu mtoni ambapo wehu wenzetu huko Musoma unywa maji yake na utumia kwa shughuli mbalimbali kwani maji ni uhai. Sisi kweli ni wema kwani hayo tumeyafumbia macho.

Hawa wehu wenzetu wanawachekesha sana, eti mtu kushika chaki anawapigia kelele, anawakondesha, yaani kwao ni maajabu sana. Waache kwenda ulaya kusaini uuzaji wa vifaa vya basi letu wawawezeshe wehu washika chaki? Waache kula kuku kwa mrija na kugonga glasi za mvinyo wamjengee mshika chaki nyumba nzuri ya kuishi? Wametufunga midomo tukafie mbali, kushika chaki tunataka hali nzuri ya nini? Nani tunamfaidisha? Kwanza waonavyo ni bora tusipewe chaki bali mkaa ili wapate vinono na kwenda kujenga mahekalu ya kuvutia na ya kupendeza ili wao na familia zao waishi maisha ya peponi, wehu tukizidi taabika.

Wamekaa kimya wakiwangalia wehu wenzetu, wehu wanaojiita wafanyakazi, kwamba nao wanajisumbua kupanga mgomo, wanatusihi tuwasemeshe, hawajui watendalo. Sisi kweli tumekaa kimya wehu wenzetu wapambane kivyao vyao mana kila mtu atauchukuwa mzigo wake. Wehu wenzangu, siku ya siku tutakuwa mashahidi. Wehu wenzetu wataburuzwa na virungu na kukiona cha mtema kuni kana kwamba ni wavamizi ndani ya basi letu.

Mwehu mwenzangu. Tulio wapa udereva na ukonda wamekaa juu ya basi letu wakila vyuku na bia, wanatucheka jinsi walivyo tuburuza Mwanzo wa msimu mpaka hapa tulipo. Wanajiandaa omba nafasi ya kutuongoza na kuliendesha basi letu kwa mara nyingine. Wanajisifu kwamba kwa kanga, kofia, t-sheti na wali tutawachagua tu. Mie najua ni wehu tulionao ndio utatupelekea tuwape nafasi nyingine ya kutuburuza na kutuacha taabani na basi letu. Wanatuambia tusichoke, tuwachague tena sisi wehu ili tuendelee kula msoto, ukondoo wetu ndio chanzo cha wao kutuburuza.

Wanatusihi tusikose siku ya kuchagua, ewe mwehu mwenzangu uwahi mapema kufika kituoni na umchague bila shaka mwizi na dereva asiye na utambuzi wa nini cha kukufanyia ili kukuokoa katika mchoko na uchovu ulio nao na akuburuze kwa hali ileile na kasi ileile.


MAGIC HOUSE BY STEVEN KANUMBA


it`s kanumba again with MAGIC HOUSE,


STARING : KANUMBA a.k.a the great, Nagris Mohamed
MOVIE : MAGIC HOUSE
PRODUCTION/STUDIO : GAME 1st QUALITY
SCRIPT : STEVEN KANUMBA
COUNTRY : TANZANIA
LANGUAGE : SWAHILI


BUY IT!
WATCH IT NOW!

afrotanza gallery